• HABARI MPYA

    Monday, June 09, 2014

    MAREKANI YAICHAPA NIGERIA 2-1, SASA YAENDA BRAZIL KIFUA MBELE

    MABAO mawili ya Jozy Altidore jana yameipa Marekani ushindi wa 2-1 dhidi ya Nigeria katika mchezo wa mwisho wa kujiandaa na Kombe la Dunia Uwanja wa EverBank Field mjini Jacksonville.
    Altidore alimaliza ukame wa mabao ndani ya miezi sita kwa klabu na timu yake ya taifa kwa kufunga bao moja kila kipindi na kuifanya Marekani iende Brazil ikitoka kushinda mechi tatu mfululizo za kirafiki.
    Alifunga: Jozy Altidore, kushoto, alifunga mabao tote mawili Marekani ikiilaza 2-1 Nigeria

    Mshambuliaji wa Nigeria, Victor Moses alizima matumaini ya Tim Howard kumaliza mechi bila kufungwa katika mchezo wake wa 100 akiifakia Marekani baada ya bao la dakika za lala walama kwa penalti.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAREKANI YAICHAPA NIGERIA 2-1, SASA YAENDA BRAZIL KIFUA MBELE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top