Beki wa kulia aliyeitwa hivi karibuni timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Hassan Ramadhani Kessy akijifua na kikosi cha timu hiyo kambini Johannersburg, Afrika Kusini kujiandaa na mchezo dhidi ya Algeria Novemba 14, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na marudiano Novemba 17 mjini Algiers. Kessy anayechezea Simba SC na Juma Abdul wa Yanga SC, wote wameitwa katika nafasi ambayo Shomary Kapombe wa Azam FC ndiye chaguo la kwanza. |
0 comments:
Post a Comment