SIMBA SC YAMSAJILI BEKI NASSOR KAPAMA WA KAGERA SUGAR
KLABU ya Simba imemtambulisha beki Nassoro Kapama kutoka Kagera Sugar kuwa mchezaji wake wa nne mpya kuelekea msimu ujao. Kapama anakuwa mzawa wa pili mpya kusajiliwa Simba baada ya mshambuliaji Habib Kyombo kutoka Mbeya Kwanza iliyoshuka Daraja. Wengine ni kiungo Mnigeria, Victor Akpan kutoka Coastal Union na mshambuliaji Mzambia, Moses Phiri kutoka Zanaco ya kwao.
0 comments:
Post a Comment