• HABARI MPYA

    Saturday, June 02, 2012

    AZAM YAIPA ONYO LA KIUNGWANA SIMBA SC

    KLABU ya Azam FC, imesema kwamba inachezea rungu la Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa kutaka kumsajili kihuni mchezaji wao, brahim Rajab Jeba.
    Meneja wa Azam FC, Patrick Kahemele ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, Jeba anatoka kwenye kituo cha kulea vipaji cha Azam FC na inakumbukwa kilichowakuta Chelsea baada ya kumsajili Gael Kakuta kinyemela licha ya kwamba, mchezaji huyo hakuwa na mkataba na klabu ya RC Lens ya Ufaransa lakini FIFA iliwatia hatiani Chelsea na kuwaamuru wailipe Lens
    "Tafsiri yake ni kuwa wachezaji waliolelewa kwenye Academy hata bila mikataba hufungwa na ile klabu ilyomlea ndiyo maana pesa ya TP Mazembe kwa Samata ilifika Mbagala kwenye kituo kilichomlea,"alisema Kahemele na kuongeza
    "Pili kwa kuwa Ibrahimu Jeba, ambaye Azam ilimtoa kwa mkopo msimu uliopita kwa klabu ya Villa Squad bado ana mkataba na Azam.
    "Kitendo cha Simba kufanya naye mazungumzo na kumhamisha kinyemela ni uvunjifu wa kanuni za soka zilizowekwa na halitofautiani na tukio la Chelsea kuzungumza na Ashley Cole nje ya wakati wa usajili, tukio lililoifanya FA wakati huo iwape adhabu Chelsea,"alisema Kahemele.
    Simba inataka kumsajili Jeba kama mchezaji wa Villa Squad iliyoshuka daraja Ligi Kuu na tayari ameanza mazoezi ya awali na Wekundu hao wa Msimbazi katika gym.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM YAIPA ONYO LA KIUNGWANA SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top