• HABARI MPYA

    Monday, June 11, 2012

    PIGO SIMBA, CHOLLO KUTOCHEZA KAGAME, AUMIA KAMA UHURU NA OWINO


    Chollo

    BEKI wa kulia wa Simba SC, Nassor Masoud ‘Chollo’ atakuwa nje ya Uwanja kwa wiki sita, kufuatia kuumia kwake katika mazoezi ya timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wiki mbili zilizopita timu hiyo ikijiandaa na mechi na Ivory Coast.
    Daktari wa Simba SC, Cossmas Kapinga ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba baada ya kufanyiwa vipimo, imebainika Chollo anatakiwa kuwa nje ya Uwanja kwa wiki sita, jambo ambalo litamfanya akose hadi michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
    Kapinga alisema kwamba Chollo ameumia mfupa wa katikati ya goti, kama walivyoumia beki wa zamani wa Simba, Mganda Joseph Owino ambaye kwa sasa yupo Azam FC na kiungo wa timu hiyo, Uhuru Suleiman ambao wote walilazimika kuw anje ya Uwanja wa msimu mzima.
    “Tofauti yake Chollo na akina Owino ni kidogo sana, yeye (Chollo) haujavunjika wote, lakini wenzake ulivunjika wote, pamoja na yote wiki sita ni nyingi. Anaweza asionekane kanisa uwanjani mwaka huu, kwa sababu hadi apone aanze taratibu, ni mtihani,”alisema Kapinga.
    Kuumia kwa beki huyo si pigo kwa klabu yake tu, bali hata kwa Taifa Stars, kwani Chollo amekuwa chaguo la kwanza kote huko.    
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PIGO SIMBA, CHOLLO KUTOCHEZA KAGAME, AUMIA KAMA UHURU NA OWINO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top