Winga wa Yanga, Geoffrey Mwashiuya (kulia) akimtoka kiungo wa African Lyon, Abdallah Mguhi 'Messi' katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 1-1
Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe akituliza mpira kifuani katikati ya wachezaji wa Lyon
Mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Martin akienda kupiga mpira kichwa dhidi ya Abdallah Mguhi wa Lyon
Abdallah Mguhi akipiga mpira mbele ya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima
Kiungo wa Yanga, Thabani Kamusoko akikosa bao la wazi jana
Mshambuliaji wa African Lyon, Thomas Maurice (kushoto) akimiliki mpira mbele ya beki wa Yanga, Vincent Bossou
Beki wa Lyon, Miraj Adam (kushoto) akimdhibiti winga wa Yanga, Deus Kaseke
Beki wa Yanga, Mwinyi Hajji Mngwali (kulia) akitafuta maarifa ya kumpita beki wa Lyon, Bakari Jaffar
Mkurugenzi wa Ufundi wa Yanga, Mholanzi, Hans van der Pluijm (kushoto) akizungumza na kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa wakati mchezo huo ukiendelea jana
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba (katikati) akifuatilia mchezo wa jana kwa umakini kabisa
0 comments:
Post a Comment