MAKAMU wa rais wa zamani wa Chama cha Soka China,
amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, kwa kukutwa na hatia ya rushwa na
upangaji matokeo.
Taarifa ya Shirika la Habari China, Xinhua, imesema Yang Yimin amekutwa na hatia ya kujipatia hongo ya yuan Milioni 1.25 (sawa na dola za Kimarekani 200,000) na kutupwa jela kuanzia jana hadi miaka kumi na nusu.
Mwenzake Yang, kutoka Kamati ya Marefa, Zhang Jianqiang, pia alitupwa jela miaka 12 kwa kukutwa na hatia ya kuchukua hongo ya yuan Milioni 2.73 (dola 433,000).
Refa Lu Jun, aliyechezesha mechi mbili katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2002 Korea Kusini na Japan, alihukumiwa kifungo cha miaka mitano na nusu Alhamisi kwa kupokea rushwa ya dola 130,000 kupanga matokeo ya mechi saba za ligi.
Taarifa ya Shirika la Habari China, Xinhua, imesema Yang Yimin amekutwa na hatia ya kujipatia hongo ya yuan Milioni 1.25 (sawa na dola za Kimarekani 200,000) na kutupwa jela kuanzia jana hadi miaka kumi na nusu.
Mwenzake Yang, kutoka Kamati ya Marefa, Zhang Jianqiang, pia alitupwa jela miaka 12 kwa kukutwa na hatia ya kuchukua hongo ya yuan Milioni 2.73 (dola 433,000).
Refa Lu Jun, aliyechezesha mechi mbili katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2002 Korea Kusini na Japan, alihukumiwa kifungo cha miaka mitano na nusu Alhamisi kwa kupokea rushwa ya dola 130,000 kupanga matokeo ya mechi saba za ligi.



.png)
0 comments:
Post a Comment