SOTO ALIVYOANZA KUMREJESHA KAZINI KAPOMBE TARATIBU LEO CHAMAZI
Mtaalamu wa viungo wa Azam FC kutoka Hispania, Sergio Perez Soto akimfanyisha mazoezi beki wa timu hiyo, Shomary Kapombe asubuhi ya leo kwenye gym ya klabu hiyo ndani ya viunga vya Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam
Kapombe ameanza mazoezi leo baada ya kuwa nje ya Uwanja tangu Aprili kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa Pulmonary Embolism (donge la damu kuziba mishipa ya damu katika mapafu).
Kapombe sasa anapambana ili kuwa fiti aweze kurejea uwanjani msimu ujao
Leo ameanza taratibu mazoezi ya gym na atakuwa akiongeza kasi taratibu kadiri siku zinavyokwenda
0 comments:
Post a Comment