WENYEJI, Dodoma Jiji FC wamelazimishwa sare ya bila mabao na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida.
Kwa matokeo hayo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 25 na inabaki nafasi ya nane ikiendelea kuizidi pointi mbili Namungo FC inayosaliia pia nafasi ya tisa katika ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 20.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.



.png)
0 comments:
Post a Comment