Mshambuliaji Mfaransa anayetakiwa na Manchester United, Antoine Griezmann akishangilia baada ya kuweka rekodi mpya ya kuwa mchezaji aliyeifungia mabao mengi zaidi kwenye michuano ya Ulaya, klabu yake ya sasa, Atletico Madrid ya Hispania kufuatia kufunga bao moja usikku wa jana dakika ya 25 katika ushindi wa 4-2 dhidi ya wenyeji, Bayer Leverkusen Uwanja wa BayArena, Leverkusen, Ujerumani kwenye mchezo wa kwanza hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mabao mengine ya Atletico yalifungwa na Saul Niguez Esclapez dakika ya 17, Kevin Gameiro dakika ya 58 kwa penalti na Fernando Torres dakika ya 86, wakati ya wenyeji yalifungwa na Karim Bellarabi dakika ya 48 na Stefan Savic dakika ya 67 kwa penalti PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Where to watch Dallas Wings vs. Indiana Fever: Live stream, start time, TV
channel for Saturday, May 9
-
Caitlin Clark and the Fever open the season against the Wings.
12 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment