• HABARI MPYA

    Saturday, May 09, 2026

    NDUWUMWE AFUNGA TENA MAWILI SINGIDA BLACK STARS YAITANDIKA MTIBWA SUGAR 4-0


    TIMU ya Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida.
    Mabao ya Mtibwa Sugar yamefungwa na mawinga, Mrundi Mossi Nduwumwe, mawili dakika ya 10 na 42, Mgambia Gambia Lamine Jarjou dakika ya 52 na kiungo Mghana, Emmanuel Kwame Keyekeh  dakika ya 67.
    Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 35 na kurejea nafasi ya nne ikiizidi pointi mbili TRA United  baada ya timu zote kucheza mechi 22, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 23 za mechi 22 pia nafasi ya 11 kwenye ligi ya timu 16.
    Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
    Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NDUWUMWE AFUNGA TENA MAWILI SINGIDA BLACK STARS YAITANDIKA MTIBWA SUGAR 4-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top