TIMU ya Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Airtel Mwigulu mjini Singida.
Mabao ya Mtibwa Sugar yamefungwa na mawinga, Mrundi Mossi Nduwumwe, mawili dakika ya 10 na 42, Mgambia Gambia Lamine Jarjou dakika ya 52 na kiungo Mghana, Emmanuel Kwame Keyekeh dakika ya 67.
Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 35 na kurejea nafasi ya nne ikiizidi pointi mbili TRA United baada ya timu zote kucheza mechi 22, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 23 za mechi 22 pia nafasi ya 11 kwenye ligi ya timu 16.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.



.png)
0 comments:
Post a Comment