TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania imefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Michuano ya Futsal Afrika baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Senegal kwenye mchezo wa mwisho wa KUndi C jana Uwanja wa Salle Moulay Abdellah Jijini Rabat nchini Morocco inakofanyika michuano hiyo.
Mabao ya Tanzania yalifungwa na Donisia Minja dakika ya 13, Vaileth Nicholas Mwamakamba dakika ya 20 na Anna Katunzi dakika ya 21, wakati la Senegal lilifungwa na Ndeye Kane dakika ya 29 - na sasa itamenyana na Morocco kesho kuanzia Saa 2:00 usiku hapo hapo Salle Moulay Abdellah Jijini Rabat.
0 comments:
Post a Comment