TANZANIA imeanza vibaya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya Umri wa miaka 20 baada ya kuchapwa bao 1–0 na Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi A leo Uwanja wa Suez Canal Jijini Ismailia nchini Misri inakofanyika michuano hiyo.
Bao pekee la Amajita lililoizamisha Ngorongoro Heroes limefungwa na Shakeel April wa Cape Town City dakika ya 27 akimalizia kazi nzuri ya Mogamat Faiz Abrahams wa Stellenbosch, wote viungo.
Ngorongoro Heroes itashuka tena dimbani Mei 3 kumenyana na Sierra Leone, kabla ya kucheza na Zambia Mei 6 na kukamilisha mechi zake za Kundi A Mei 9 kwa kumenyana na wenyeji, Misri.
0 comments:
Post a Comment