Mshambuliaji Mfaransa kinda wa umri wa miaka 20, Kylian Mbappe akishangilia baada ya kuifungia Paris Saint-Germain bao la pili dakika ya 60 kufuatia Presnel Kimpembe kufunga la kwanza dakika ya 53 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Manchester Uinited Uwanja wa Old Trafford kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana. Huo unakuwa mchezo wa kwanza Man United ambayo ilimaliza pungufu baada ya kiungo wake, Paul Pogba kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 89, kupoteza chini ya kocha mpya wa muda, Ole Gunnar Solskjaer PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Will McLaren be worried about Norris-Piastri relationship?
-
BBC Sport F1 correspondent Andrew Benson answers your latest questions
following the Hungarian Grand Prix.
30 minutes ago
0 comments:
Post a Comment