Wachezaji wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars wakiingia uwanjani kwa ajili ya mchezo wa Kombe la CECAFA Challenge dhidi ya Zambia Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza mwaka 1992. Stars ilifungwa 2-1 licha ya kutangulia kwa bao la Edibily Lunyamila dakika ya 11, Kelvin Mutale akasawazisha dakika ya 33 na kufunga la ushindi dakika ya 56. Stars iliokuwa Kundi B ilitolewa baada ya kushika nafasi ya tatu nyuma ya Malawi na Zambia, zilizofuzu Nusu Fainali. Timu nyingine katika kundi hilo, zilikuwa Zanzibar na Ethiopia. Timu B ya Tanzania, Kakakuona iliyokuwa Kundi A Arusha, ilifika hadi fainali na kufungwa na 1-0 na Uganda, bao pekee la Issa Sekatawa dakika ya 77.
CALUM McCLURKIN: Chester chaos presents plenty of grounds for concern in a
week filled with farce
-
The May election for the Scottish Parliament were labelled 'the Meh'
elections this week due to the level of public disillusionment with
politics in Holyrood.
43 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment