• HABARI MPYA

    Sunday, May 18, 2025

    YANGA SC YATINGA FAINALI KOMBE LA CRDB


    MABINGWA watetezi, Yanga SC wamefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Tanzania jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    Mabao ya Yanga leo yamefungwa na mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 41 na kiungo mzawa, Mudathir Yahya Abbas dakika ya 89.
    Yanga sasa itakutana na mshindi wa Nusu Fainali ya pili, Singida Black Stars na Simba zitakazomenyana baadaye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC YATINGA FAINALI KOMBE LA CRDB Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top