• HABARI MPYA

    Tuesday, May 06, 2025

    BODI YATOA RATIBA MPYA; SIMBA NA YANGA NI JUNI 15 ‘KWA MKAPA’

    BODI ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imetoa ratiba ya kukamilisha msimu huku mchezo wa watani wa jadi, Simba SC na Yanga ukipangwa kufanyika Juni 15 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
    Awali mchezo huo ulipangwa kufanyika Machi 8, lakini Simba wakagoma kwa madai walizuia na wenyeji, Yanga kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa siku moja kabla ya mechi kwa muiibu wa kanuni.


    Yanga iliandika malalamiko TPLB ikiomba ipewe ushindi baada ya Simba kutotokea uwanjani — na baadaye wakapeleka malalamiko Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo (CAS) wakiomba pia wapewe ushindi.
    Lakini FIFA na CAS wakaitaka kwanza Yanga ianzie kwenye mamlaka za nchini — lakini jana klabu hiyo imetoa taarifa ya kusistiza kutocheza mechi hiyo kwa sababu hawana imani na mamlaka za nchini.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BODI YATOA RATIBA MPYA; SIMBA NA YANGA NI JUNI 15 ‘KWA MKAPA’ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top